Translate

Friday, May 12, 2017

MKUU WA MKOA WA GEITA AZINDUA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI KWENYE MIRADI MITANO!



Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenereli  Mstaafu Ezekiel Kyunga amezindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi mitano ambapo mitatu ni vituo vya afya na viwili ni shule moja na Mabweni kwenye shule ya sekondari Kasamwa.

Akielezea Miradi hiyo yote Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji  Mhandisi Modest Aporinali  amesema bajeti ambayo waliyonayo kwa kila kituo cha afya wametenga kiasi cha sh ,Milioni Mia moja na kwamba mahitaji ni vituo vya afya kumi na kwasasa ni vituo viwili ambavyo vinafanya kazi.

“Ni kweli Halamshauri yetu ina uhitaji mkubwa sana wa Vituo vya afya ingawa kwa sasa tunavyo vituo viwili ambavyo ni Nyankumbu na Kasamwa ambavyo vinafanya kazi, hata hivyo mmeona tumezindua na kuweka mawe ya msingi kwenye vituo vitatu ambapo ni Mpomvu,Nyanguku na Shiloleli tutaendelea na jitihada kwa kutumia mapato yetu ya ndani ili kupunguza changamoto ya vituo vya afya hata hivyo GGM wametupa msaada kama milioni mia moja kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya Mgusu”Alisema Modest. Picha kwa hisani ya Madukaonline

No comments:

Post a Comment